CHAMA cha Waandishi wa habari wanawake Zanzibar(TAMWA) kimetoa mafunzo maalumu ya uongozi kuanzia tarehe 20,21 na 22 kwa upande wa Unguja ndani ya mwezi huu wa Machi 2023 kwa wagombea wanawake watarajiwa kutoka vyama mbalimbali vya siasa vya Zanzibar.
Mafunzo
hayo yamejumuisha vyama nane 08 vya siasa
vilivyopo unguja ikiwemo chama
cha CCM, ACT Wazalendo, CHADEMA , CUF, ADC, ADA TADEA, UMD,UDP pamoja na
viongozi mbalimbali wa Vyuo Vikuu kwa lengo la kuwajengea uwezo wanawake hao
kiuongozi wakati wa uchaguzi, ikiwa ni miongoni mwa utekelezaji wa majukumu na
malengo ya mradi wa SWILL(Strengthen Women In Leadership) wa kuinua wanawake
katika uongozi.
Akifungua
mafunzo hayo Mkurugenzi wa Chama Cha Waandishi Wa Habari Wanawake Zanzibar
(TAMWA) Dkt Mzuri Issa amewataka viongozi hao kuwa na ujasiri, uthubutu na
utayari katika kugombea nafasi za uongozi kwenye nyadhifa yeyote ile ili kuleta maendeleo bora kwenye shehia,
majimbo na hata mikoa. “Kama wanawake tuna haki zote za kugombea nafasi yeyote ya uongozi ili kuleta
maendelea chanya katika nchi yetu” alisema Dkt Mzuri Issa.
Nae
Maryam Ame Chum mratibu wa mradi wa kuinua wanawake katika uongozi ameeleza
lengo la mafunzo hayo ya uongozi kwa wagombea wanawake watarajiwa kuwa “
jumla ya wanawake 80 tumekusudia kuwapa mafunzo ya uongozi kati ya hao
45 kutoka Unguja na 35 kutoka Pemba kwa lengo la kuwajengea uimara kwenye
harakati za kiuongozi”
Miongoni
wa wakufunzi walioweza kuhudhuria na kutoa mafunzo kwa waombea wanawake
watarajiwa ni Lutfia Faida Haji ambae ni Afisa jinsia katika kitengo cha Jinsia
na Mjumuisho wa Jamii kutoka tume ya uchaguzi Zanzibar kwa lengo la kutoa
utaratibu na mwongozo kwa wagombea watarajiwa katika zoezi la kujaza fomu za
kugombea wakati wa uchaguzi kwa
utaratibu unaotakiwa. “kwa mujibu wa sharia za Tume Ya Uchaguzi Ya Zanzibar
hakuna pingamizi yeyote kwa mwanamke kuingia katika kinyanganyiro cha uongozi
ikiwa atatimiza sifa za kugombea na kuchaguliwa” alisema Afisa Jinsia na
Mjumuisho wa Jamii. Pia aliongeza kwa kusema “kifungu cha 35 katika sheria ya
uchaguzi ya Zanzibar kimetoa fursa kwa wanawake kuwa baraza la wawaikilishi
linafikisha asilimia 40 ya nasafi za uongozi kwa wanawake”
Pia
Mwanaidi Suleiman Ali ambae ni Afisa wa Uhusiano ZAECA aliweza kuwapa elimu
wanawake hao juu rushwa ya ngono na kuwaeleza juu ya jitihada za mapambano zidi
ya rushwa Zanzibar ambapo sheria ya kuzuia rushwa ilitungwa mwaka 1975 na mwaka
2012 ilipitishwa na Baraza La Wawakilishi Zanzibar. “kuna aina nyingi za rushwa
lakini rushwa hii ya ngono imepewa nafasi kubwa na ndio ndio mbaya zaidi, hivyo
mkiwa mnaelekea kwenye uchaguzi wa vyama vyenu ni lazima mkubali kubadiika na
kukataa kudhalilika ili kulinda hadhi yako ya ujanajike” alisema Afisa Uhusiano
ZAECA.
Naima
Salum Hamadi kutoka chama cha UDP alieleza kuwa “katika uchaguzi wa 2020
niligombea nafasi ya Spika wa Baraza la Wawakilishi kupitia tiketi ya chama changu cha UDP lakini sikubahatika
kushinda ila kupitia mafunzo haya niliyoyapata yamenijengea uwezo hata 2025
nije kugombea tena panapo uhai na uzima.”
Pia
Khayam Mustafa Yakuti kutoka Chama Cha Mapinduzi(CCM) alieleza kuwa “ kwa sasa
nina nafasi ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi
(UVCCM) katika jimbo la Malindi na
nashkuru kupatiwa mafuzo haya ya uongozi kutoka TAMWA kwani yameniongezea hamasa
na kunifanya nijione kuwa natosha kugombea nafasi yeyote ile ya uongozi iwe ya
serikali au ndani ya chama”
Nae
Yusra Khalid Kombo kutoka chama cha ACT Wazalendo alieleza kuwa “ mimi niliwahi
kugombea nafasi ya Udiwani katika wadi ya Mwanyanya jimbo la Mtoni mwaka 2020
kwa kuamini ninaweza na kupitia mafunzo haya yameniongeza ari zaidi ya kuja
kugombea tena kwenye uchaguzi wa 2025”
Pia
Hudhaimat Kheri Salim ambae ni Makamu Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyuo Vikuu na
taasisi za elimu ya juu Zanzibar (ZAHILFE) alieleza kuwa “kwa niaba ya viongozi
wenzangu wa vyuoni tutahakikisha mafunzo haya ya uongozi tuliopatiwa na TAMWA
tunayetendea haki katika nafasi zetu za uongozi na pia tutakuwa mabalozi wazuri
kwa wanafunzi wengine”
Kwa
kumalizia, nae mmoja wa wakufunzi wa mafunzo hayo ya uongozi Dkt Salim Suleiman
Ali aliwasisitiza viongozi hao kujuwa haki zao uongozi katika mchakato wa
demokrasia pamoja na kutumia teknolojia ya habari itakayoweza kuwasaidia
wanawake katika siasa na kutimiza malengo yao ya uongozi.


0 Comments