HABARI MPYA

6/recent/ticker-posts

Sakina Khamis Mwanamke Shupavu alieitumia Pesa ya TASAF kutoka kwenye Umasikini

 


Na Essau Kalubila.

‘’MIMI sasa sijioni mwanamke, najiona kama mwanamme mwenye uwezo mkubwa, ndio maneno ya mwanzo wa mlengwa kaya maskini Sakina Khamis Mbwana miaka (37), wa Shehia ya  Tumbe Mashariki Pemba Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Nilipotaka kujua kwanini asijifananishe na mwanamke aliyepata mafanikio, kwanza aliagusha kicheko na kusema, ameshahama kwenye uwanawake kiuwezo, na sasa ni sawa na mwanamme.

Nilipomng’ang’ania sababu za kujifananisha na mwanamme, alisema ilishazoeleka na kuaminika kuwa mwanamke hawezi kwa na mafanikio.

KABLA YA KUFIKIWA NA TASAF

Sakina kwa bahati mbaya, mwaka 2013 alifiliwa na mume wake, aliyemuachia watoto sita, wakati huo wakiishi kwenye nyumba ya miti na makuti.

Matunzo ya watoto hao, anakumbuka kuyapata ndani mwezi mmoja, baada ya kufiliwa na muumewake, ingawa kuanzia hapo, hakuna tena mchango hata wa kupata majani ya chai kutoka kwenye familia.

Hadithi ikawa kwake yeye ni mgagaa na upwa hali ugali mkavu, ingawa baadhi ya siku, akiukosa hata huo mkavu kula na watoto wake sita mayatima.

Haki ya elimu kwa watoto, ilikuwa ni ya kusua sua, mara wasimamishwe mara waruhusiwe kutokana na kutokuwa na uhakika wa mchango hata wa shilingi 100.

Baada ya kuondokewa na mume wangu, kazi sasa ilikuwa ni kuuza maandazi na maziwa eneo la soko la samaki Tumbe, ingawa kipato kilikuwa kidogo.

‘’Nikimaliza bidhaa hizi, ilikuwa faida haizidi shilingi 4000, wakati ndani nina watoto sita, wanaohitaji mlo wa asubuhi pekee ni shilingi 6,000 kwa siku,’’anasema.

Alikuwa akimaliza bidhaa hiyo, miguu yake huelekea baharini kuungana na wenzake, kwenye kilimo cha mwani ambapo kwa wakati huo, kilo mmoja mkavu ni shilingi 700.

Hata alipojiunga kwenye kilimo cha mwani, anasema hakumbuki hata siku moja, watoto wake waliokula wakibakisha chakula kwenye dishi.

‘’Mimi ili nishibe vyema na watoto wangu, kuanzia asubuhi hadi jioni, ilikuwa nahitaji shilingi 1,5000 kwa siku, ingawa nilikuwa natimiza shilingi 5000,’’anasimulia.

Sakina hakumbuki watoto wake kuvaa nguo mpya hata siku za sikukuu, na siku moja baada ya kukosa cha kuvaa, aliwatembeza watoto wake soko la samaki Tumbe, baada ya kukosa hata nguo za mtumba.

‘’Wao hawakujua kwa sababu gani, tunakwenda kutembea sokoni, badala ya eneo letu la kusherehekea sikukuu, lakini ilitokana na kukosa nguo,’’anasilimulia.

Hakuwa na ndoto hata siku moja, kupata chakula cha kutosha, kutimiza ada ya skuli ya watoto wake, au kufikia sikukuu wakavaa nguo za dukani kama wenzao.

BAADA YA UJIO WA TASAF

Sakina anakiri kuwa, hakuamini alipoitwa na sheha wake, juu ya kurodhesha majina ya watoto wake, na taarifa nyingine za maisha, akiona kama ni mchezo.

Alikuwa na hakika kuwa, hakuna mpango wa kunusuru kaya maskini, ambapo anaweza kulipwa fedha na pasi na kufanya kazi.

‘’Ukishakuwa na watoto yatima na hali yako ikiwa ya kinyonge, atakuja huyu kukuandika, yule kukupiga picha na kisha mwisho wa siku, hakuna jambo,’’anakumbuka.

Baada ya TASAF kuitia roho na kuitwa jina lake kwa ajili ya kupokea, hakuamini moyo, macho na hisia zake kuwa amepata ruzuku hiyo.

‘’Siku ya mwanzo nilipokea shilingi 48,000 na nilielezwa ni kwa ajili ya watoto, iwe katika elimu ya skuli au huduma za afya, na hapo ndio nikaanza kuamini,’’anasema.

Sakina ambae yumo kwenye wale walengwa 14, 280 wa Pemba kuanzia mwaka 2014 hadi mwaka 2019, anakumbuka fedha hizo, hakufanya kosa na aliwanunulia vifaa vya elimu watoto wake.

Kuanzia hapo, watoto wake ilikuwa hawaendi skuli na sare mbovu, viatu visivyofahamika na hakuna siku waliyorejeshwa kwa ukosefu wa michango wa skuli.

Alidumu kwa miezi mitatu kupokea shilingi 48,000, ingawa baada ya kukiuka masharti, alipokea ruzuku ya shilingi 36,000 kutoka TASAF.

MRADI WA KUKAANGA SAMAKI

 ‘’Nikiwa napokea shilingi 36,000 sasa nikamua niende bandirini Tumbe, kununua samaki wa shilingi 10,000 kwa ajili kukukaanga na na mafuta ya shilingi 200 na baada ya kuuza, nilipata faida ya shilingi 5000,’’anasema.

Mlengwa huyo, kazi hiyo ilimgia gegoni sawa sawa, na kuanzia mwaka 2000, akawa ananunua samakini wa shilingi 45,000 hadi shilingi 50,000.

‘’Huku watoto wangu wakiwa wanakwenda skuli kama kawaida, na biashara yangu iling’aa, na sasa hadi kufikia kujipatia faida ya shilingi 15,000 kwa siku kutoka ile shilingi 5000 ya zamani,’’anasema.

 

HAPA, baada ya kujikusanyia faida hadi kufikia shilingi 50,000 huku akiendelea kuwahudumia watoto wake sita mayatima, alizaa wazo la kuanzisha genge.

Genge hili aliamua kuuza bidhaa kama tungule, bilingani, bizari, nazi ingawa halikudumu, kutokana na kutokuwa na nafasi ya kuwepo nyumbani.

‘’Asubuhi nafuata samaki sokoni Tumbe, wakati huo huo natakiwa nikafuatilie viungo vya mchuzi mjini, nikaona siwezi kujigawa, hivyo baada ya muda genge niliacha,’’anasema.

Fedha alizoanzia genge na faida anayoendelea kuipata kwenye samaki wa kukaanga, hadi inalifikia shilingi 20,000 sasa alizaa mradi mwengine.

Ingawa pembeni ya miradi hii, Sakina alikuwa akiendesha mradi mwengine, wa kununua na kuuza sabuni za karafuu, akisema mwenyewe kwa ajili ya chai ya watoto.

‘’Nilidumu nao kwa muda wa zaidi ya miaka mitatu, lakini huu ulikuwa ni baada ya saa za kazi, lakini hata navunja kisanduku mlikuwa na shilingi 200,000,’’anasema.

MRADI WA NGUO ZA MITUMBA

Hapa, faida ya sabuni ya shilingi 200,000 ndio alioanza kununua nguo za mitumba kutoka Kenya, ambapo alimtuma mtu aliyekuwa kuweko kwa shughuli za uvuvi.

‘’Kwa sasa nimeshaolewa, na mume wangu alipofika Kenya wakati anataka kurudini mwezi Disemba mwaka 2022, ndie niliemuagiza na sasa naendelea na biashara hii hapa kwangu,’’anasema.

Mara ya kwanza, alipotuma shilingi 200,000 kwa bidhaa hiyo, alijipatia faida ya shilingi 40,000 na sasa kwa mara ya pili, alituma tena shilingi 400,000 ambapo hadi mwezi huu  akiendelea kuuza.

Kwa sasa anamiliki wastani wa shilingi milioni 1 kama mtaji, na hasa baada ya kujiingiza kwenye kisanduku (kikoba), ambapo mwezi Machi mwaka 2023, alikopa shilling 300,000.

MALENGO YAKE

Tayari ameshanunua kiwanja kutoka kwa familia, na hapo baadae anajipanga kuanza ujenzi, ili aondokane na kodi ya mlango kwenye biashara yake.

Kwa sasa anaishi kwenye maisha ya ubinaadamu na furaha, na hasa baada ya kuwaona watoto wake wanaendelea na masomo.

KATIBU WA SHEHA

Katibu wa sheha wa shehia ya Tumbe Mashariki, Makame Hassan Makame, anasema wapo wananchi 20 waliomo kwenye mpango, ambao sasa wamejiongeza.

Maana shehiani hapo, kati ya wananchi 7,675 waliofikiwa na mpango wa kunusuru kaya maskini walikuwa ni 231, ingawa kwa sasa wanaoendelea ni 225, akiwemo Fatma Rubea Ali.

Wapo walioanzisha ushirika wa biashara kilimo cha mboga, ufugaji vikundi vya kuweka na kukopa.

Lakini, akasema ipo miradi kadhaa ambayo inawalenga jamii wote, kama vile ujenzi wa tuta la kinga maji, ambapo wakulima zaidi ya 45, wamenufaika.

“Wakulima 45 walishayahama mashaba yao kwa kuingia maji ya bahari, lakini TASAF ilianzisha mpango wa kujenga tatu la kukinga maji, na sasa wakulima wamerudi,’’anasema.

Akaiomba TASAF, mara itakapomalizika mpango huo kwa awamu ya kwanza, bado kwenye shehia yake, anao zaidi ya wanachi 200 wanaohitaji kunusuriwa.

MUUME WA SAKINA

Kwani hakupenda jina lake lichapishwe, ingawa anasema mke wake sasa anamuona kama mfalme kwenye maisha yake.

‘’Hata namma ya kumshirikisha kwa kila jambo langu la maisha, sasa najiona liko juu, maana amekuwa mtunza fedha na mtumiaji mzuri,’’anasema.

Kwake sasa hana wasi wasi wa huduma za ndani, maana mke wake amekuwa akitoa zaidi ya asilimia 60% ya kukamilisha huduma za kila siku.

TASAF

Mratibu wa TASAF Pemba Mussa Said, anasema wapo walengwa 14, 280 kwa Pemba, ambao wanaendelea kupata fedha za kunusuriwa na umaskini.

Walengwa hao wapo kwenye shehia 78, ikiwemo ya Tumbe Mashariki, ambapo tayari shilingi bilioni 14. 4 zimeshwafikia.

Mtu kama Fatma, ndio hasa malengo ya TASAF ya kumtoa mwananchi katika unyonge, na kumleta kwenye taa, ili nae aishi maisha mazuri.

“TASAF inaorodhesha ya zaidi ya walengwa 50,000 kutoka wastani wa walengwa 15 kila shehia, kati ya shehia 78, ambao wamenzisha miradi ya kujikwamua.

“Mtu kama Fatma wa Tumbe, Amina wa Mgogoni, Mfaki wa Kwale Gongo na Maryam wa Ukunjwi ambao hatuna shaka, hawawezi kurudi tena kwenye umaskini mzito, wanafikia 50,000 kwa Pemba yote,’’anaeleza.

Mratibu Mussa anabainisha kuwa, kwa mwaka 2014 hadi 2015 walengwa hao wa kunusuru kaya maskini, waliibua miradi ya kijamii 41, idadi iliongozeka mwaka uliofuata, kwa kufikia miradi 84.

Mwaka 2017 hadi mwaka 2018, walijukuta na miradi mengine ya kijamii 21, inayuhusisha upandaji miti kama vile Makangale, uazishwaji wa vitalu na ujenzi wa matuta ya kinga maji ya bahari Ndagoni, Kiwani, Micheweni na Tumbe.

Achia mbali idadi ya watu 50,000 waliojiwekeza wenyewe, vipo vikundi 942 vikizaa walengwa 12,000 vilivyoanzishwa, kuanzia mwaka 2014 hadi sasa.

WANANCHI WA KAWAIDA

Fatma Hamad Mkandi, wa Tumbe anasema fedha zilizoekezwa kunusuru kaya maskini, zimetumika vizuri kwa vile matunda yanaoonekana.

Hassan Haji Omar, anasema kilichobakia sasa ni tasisi nyingine kuvilea vikundi hivyo, ili walengwa wake wasirudi tena kwenye umaskini.

‘’Kwetu sisi Sakina tumeshamuona kama mwanamke mwenye uwezo mkubwa, sasa maana ruzuku ya TASAF aliitumia kama inavyotakiwa,’’anasema.

    Mwisho  

Post a Comment

0 Comments