HABARI MPYA

6/recent/ticker-posts

Bi Zawadi Amour, mwanamke aliyeishi ndoto zake za uongozi na kuzifanikisha licha ya kukabiliwa na changamoto nyingi alizopitia


UTHUBUTU naweza kusema hivyo ni moja kati njia ya kutafuta mafanikio kwa aina yoyote ile iwe kisiasa kiuchumi, kilimo kadhalika katika sawala uongozi kwa Nyanja tofaut.

Jamii nyingi hasa katika bara la afrika hawaamini kuwa mwanamke ana uweza wa kuongoza na kumuchukulia ni mtu wa kukaa nyumbani tu kulea familia kadharika majukumu ya nymbani. Na wengine huwachukulia kama chombo cha starehe.

miaka (20) iliyopita katika swala la uongozi walilichukulia kuwa ni la wanaume tuu dhana hii ikapelekea wanawake kuwa nyuma kila kitu na kuamua kujishughulisha na shughuli za nyumbani pekee.

Lakini katika karine hii ya (21) wanawake wengi wameutumia ule msemo wa KUTHUBUTU ambapo tuna shuhudia wengi wakishika nafasi mbalimbali za uongozi nchini.

Wapo wabunge na wawakilishi wanawake walio chaguliwa pia kuteuliwa kutokana na upambanaji na sasa ni wawakilishi wazuri ka majimboni mwao.

Zawad Amour Nassor ni mwanamke wa mfano alie thubutu kuingia katika siasa na kufanikiwa kuwa mwakilishi wa jimbo la konde alipambana na kuchuana na wanaume katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka?

Akizungumuza na Uga media Mh Bi Zawadi alisema kuwa kilicho mshawishi kuingia kwenye siasa ni kutokana na changamoo zilizakuwepo kwenye jamii yake kwani vinongozi walio kuwepo hawakuzitatua licha ya wananchi kukabiliwa na matatizo mengi katika jimbo lao.

Aliongeza kuwa katika utashi wake huo alopambana na vikwazo vingi kwani alianza kuvunjwa moyo kwa kuambiwa mwanamke hawezi kuongoza hasa kulingana na mjengeko wa jamii juu ya mwanamke kuwa ni mtu wa pirika za nyumba tuu,lakini kwake hakukubaliana nalo.

Je alipitia changamoto gani wakati akipambania ndoto yake?

Bi Zawadi aliongeza kuwa lilimpa changamoto kubwa kutokana na jamii nyinigi zina aamini kuwa kuingia kwenye siasa laziama uwe na pesa ila alizidi kusimama imara.


“Nilipokuwa nikiwaambia rafiki zangu kuwa nataka kugombea nafasi ya uwakilishi wafanyakazi wezangu walinitia moyo lakini kuna baadha walinivunja moyo wakisema kuwa mimi ni mwanamke siwezi kuwatetea”.

“licha ya kuwa nilivunjwa moyo wengi wao walikuwa ni wanawake na katika kura za maoni wanaume walinipa lakini wanawake wezangu hawakunipatia kura”alisema bi Zawadi.


Hata hivyo aliongeza kuwa kutokuwa na kipato hilo pia lilikuwa changamoto kubwa na kupelekea kufanya kampeni kwa mazingira magumu na kumlazimu kutembea nyumba kwa nyumba.? Haijajitosheleza..( hali ambayo iliashiria hatari hasa ukilinganisha na kutokukubalika kwake ktk jamii)

“wanasiasa wengi wamewazoesha wananchi kuwapa pesa wakati wa kampeni nami nakiti tatizo hilo lipo katika jamii kila nilipo kuwa nikipita na kufanya kampeni wananiuliza pesa utatupa niliwambia bora mnipe nafasi nichukuwe dhamana yenu ili badae mje mnidai kuliko kuwapa pesa nikipata sitowajali”

“linitamani sauti yangu ipae hasa nikiwatetea wanawake wenzangu na watoto wanao dhalilishwa hasa katika jimbo la konde lakini nashukuru sana kwakuwa sauti yangu imeanza kupaa namshukuru mungu na nitaiwakilisha vyema jamii yangu” alisema bi Zawadi.

Ni kwanamna gani aliweza kukabili vikwazo hivyo?

Licha ya kupitia vikwanzo vingi bi Zawadi aliema kuwa alisimama imara na kufanikiwa kuchukua kiti cha Uwakilishi wa jimbo la Konde na kuanza kusema kuwa nyota yake imeanza kuonekana ya kuwa kiongozi imetimia.

“Kwakweli ndoto yangu imeanza kutimia kwani tayali nimekuwa mwakilishi wa wawananchi na mafanikio yataanza kuja lakini kilicho anza kuja ni kukaa na viongozi mbali mbali na kuanza kutatua changamoto jimboni kwangu” alisema bi Zawadi.

Wanawake wanakipi cha kujifunza kwake?

Aidha hakuacha kuwasa wanawake ambao wanahitaji kuthubutu kufanya yaliomo moyoni hususan uongozi kwani msingi mkubwa ni kutokata tamaa.

#UGATvFurahaYako

 

Post a Comment

0 Comments