HABARI MPYA

6/recent/ticker-posts

KIKUNDI CHA WATU WENYE ULEMAVU WAIOMBA SERIKALI KUWAPA ENEO KUTIMIZA NDOTO YAO

Na Essau Kalukubila.
 KIKUNDI cha watu wenye ulemavu kilichopo Kiuyu Minungwini Wilaya ya Wete Mkoa Kisiwani  pemba  wametoa  kilio C hao kwa serikali wakiiomba  kuwapatia eneo  la kufanyia kazi  ili waweze kutimiza ndoto zao za kufungua kiwanda na  kutoa ajira kwa vijana wengi .

Akizungumuza na mwandishi wa habari hizi Katija Mbarock ambae ni mwanzilishi wa kikundi hicho  chenye watu 32 wakiwemo  wenye ulamavu  amesema wanafanyakazi katika  mazingira mgumu kwa kukosa eneo lakufanyia kazi zao za ushonaji  na ufumaji wa mashuka.

Aidha ameongeza kuwa licha ya viongozi  kupita katika kikundi hicho nakuona changamoto zinazowwkabali lakini bado swala la eneo halijapatiwa ufumbuzi .
 
“Tumekuwa tukipokea watu wengi na viongozi mbalimbali vyama na serikali  na kuwaeleza kwa kina changamoto zetu lakini  bado wameshindwa kutatuliwa changamoto hiy"alisema .

Aliongeza "Waziri wa ofisi ya makamu wa kwanza wa rais Zanzibar Mh Harus Said Suleiman  tulimweleza shida zetu  akatulipia mlango wa biashara muda wa mwaka mmoja na kuahidi kututafutia eneo ili tuweze kutekeleza majukumu yetu na kutumiza malengo yetu” alisema Katija.

Mmoja wa wana kikundi hicho Aisha Hamad Said mtu mwenye ulemavu wa uziwi  amesema   amekuwa akijifunza kushona na kufuma mashuka na sasa ameona furaha katika kutimiza ndoto ya kuwa mshonaji mkubwa .

Hata hivyo amewaomba wadau  mbalimbali  kuwaona kwa jicho la huruma ili waweza kutimiza ndoto zao za kufungua kiwandi ili waweza kutoa ajira ningi kwa vijana wengi Zaidi.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi ofisi ya makamu wa kwanza wa Rais Zanzibar Mh Harusi Said Suleman abae pia ni mwakilishi wajimbo la Wete amesema  tayari wapo kwenye mchakato  wa kuwatafutia eneo kujenga kitega uchumi ili waweze kutimiza malengo Yao.

Ameongeza kuwa licha ya kuwa tunapambana kutafuta eneo lingine lakini wakati huu wanaendelea  kutafutia ofisi ya kukaa kufanya kazi kwa uhuru katika maeneo ya chamanangwe.
 
“Ni kweli kikundi kile nakifahamu kwa sababu wana vijana wanapambana licha ya hali  walizonazo na    kwa kipindi hiki nipo napambana kuhakikisha wanapata ofsi  katika viwanja vya chamanangwe".alisema.

Ikumbukwe kuwa kikundi  cha UKOMBOZI WTU kilianzishwa mwaka 2020 kikiwa na wanachama  32  lengo likiwa Ni  kuwakutanisha watu wenye ulemavu na wasio na ulemavu .

Post a Comment

0 Comments