HABARI MPYA

6/recent/ticker-posts

MRADI WA KIJALUBA MKOMBOZA KWA WATU WENYE ULEMAVU

 

Na Essau Kalukubila.

KATIKA kukuza uwezo wa watu wenye ulemavu kiuchumi  kumeanzishwa vikundi vya kuweka na kukopa mabavyo vikundi hivi  vina idadi ya watu 30 kwa kila kikundi   kina watu  (20) watu wenye ulemavu na watu (10) ni watu wasio na ulemavu kwa lengo la kushilikiana.

Mafanikio haya ya kuanzisha vikundi hivi imekuja katika mradi wa KIJALUBA ambao unatekelezwa kwa muda wa miaka 2 kwa  ushirikino wa shirikisho la watu wenye ulemavu (SHIJUWAZA) na Chama cha Wandishi wa Habari wanawake Tanzania, TAMWA Zanzibar ambapo mradi huu ni wamajaribio  na unatakelezwa  kwa kipindi cha miaka miwili kwanzia mwaka 2022 hadi mwaka 2024

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Bi Husina Hamadi Ali Mwenyekiti wa kikundi cha Tukiwezeshwa tunaweza  amesema tangu kuanzisha kwa vikundi hicho yeye amekuwa  akipata faida nyingi ikiwemo  ya kukusanyika kwa kubadirishana mawazo na  kupata pesa kwa njia  ya kikundi kuweka na kukopa

Ameongeza kuwa kwamiezi iyayo kikundi chao kitakuwa na faida kubwa kutokana na wanakikundi hicho kukipenda  na kufuata mashariti ya kuweka na kukopa  nakufanya kikundi hicho kusonga mbele

“matarajio yatu katika kikundi nikukusanya pesa zikiwa nyingi tugawe ili tujiendeleze katika maisha yetu ambayo tulikuwa tumekata tamaa lakini sasa mwanga umeanza kuonekana katika maisha yetu kwakuanzishiwa kikundi hichi cha kuweka na kukopa” alisema Bi Husina

Shamkubwa Hamisi ni Mtu mwenye ulemavu wa viungo na nimama mwenye watoto wawili  lakini yeye anasama flaraha imerejea kwake baada ya  kuanzisha kikindi cha kuweka na kukopa ivisasa tayari ameanza ujasiliamari wa kushona mashuka na kuyauza na hii nikutokana na kupata pesa  kwenye kikundi chao.

Licha ya kuanzisha ujasirilimali wa kushona mashuka bado anakabiliwa na nchngamota ya vifaa kama vile chelehani ya kushonea mashuka halii imekuwa ikipelekea kwenda kuazima kifaa hicha anapo pata mteja.

“nimekuwa mbunifu wa kushona mashuka  lakini nimekuwa nikikosa chelehani hali ambayo  inanipelekea kuazima kifaa hicho  ninapo pata mtaja wa shuka  lakini nikiwa na kifaachangu maisha yangu yatabalika kabisha kwana  mashuka nauza kwa bei nzuri tu” alisema Shamkubwa  

Hadia Khamis Hilali ni mwanakikundi wa tukiwezeshwa tunaweza yeye ananiambia  awali alikuwa mjariamali  wa kusua sua  lakini baada ya kujiunga na  na kikundi hicho faida nyinga amezipata kutokana na kukopa nakuonngeza mtaji wake.

“Biashara yangu inazidi kukua siku hadi siku  na kutokana na kikikdi hiki nimekuwa nikikopa na kurudisha  mwanzo lilikopo elfu hamsini Tshg (50,000) nikarudisha nasasa nimekopa Lakimoja na Elfu Hamsini Tshg (150,000) pesahii nanunulia urembo na manukato nazunguka mtaani kuuza na faida Napata  alisema Hadia

Kwa upanda wake Mohamed Salium Khamis ni afisia mradi, mradi wa Kijaluba kutoka Chama cha wandishi wa Habari  Tanzania TAmwa Zanzibar  ofisi ya pemba amesema kuwa Mradi wa kijaluba ni mradi jumuishi  unaolenga kuwawezesha watu wenye ulemavu kiuchu, kuwajengea uwezo watu wenye ulemavu  kuhusu maisha  yao wenyewe pamoja na jamii.

Ameongeza kuwa katika kikondi kimoja kina idadi ya watu 30 kati ya hao 20 ni watu wenye ulemavu na 10 niwatu wasio na ulemavu wamekwa hao ili pale penye changamoto  waweza kuwasaidia

Akitowa wito kwa vikundi hivyo ya kuweka na kukopa amesema nivyema kufuata sharia zilizo wekwa  huku mradi huo ukiangalia namna ya kuanzisha biashara ya pamoja katika kila kikundi ambacho imejipangia kutekeleza

 

 

 

Post a Comment

0 Comments