VIFAA vyenye thamani zaidi ya
milioni mbili vimetolewa na mbunge wa viti maalumu Mkoa wa Kusini Pemba
Mhe Maryam Azani Mwinyi ikiwemo mashine ya maji, matofauti na vifaa
vyengine vya kujifunzia ili kukabiliana na changamoto ya upungufu wa vifaa
muhimu kwa wanafunzi katika baadhi ya skuli ya Mkoa huo
Mapema mbunge huyo amezi tembelea
skuli nne (4) Skuli ya Michakainia,Skuli ya Maadnalizi Madungu
Skuli ya sekondar Kilindi kwa lengo la kujua changamoto zinazo
patikana .
Akikabidhi mashine ya Maji ,
Matofali Elfu moja , mifuko arobaini (40) ya Saruji , Manila ya
kufundishia watoto na ndoo za kuhifadhia uchafu amesema kuwa
ataendeleza kutatua changamoto na sasa ameanza katika sekta ya
elimu
Afisa Mdhamini Wizara ya Elimu na
Mafunzo ya Amali Pemba Mohammed Nassor Salim
amefurahisha na mbunge kwa kutatua kero katika skuli hizo
huku Katibu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Kusini Pemba Mohamed
Ali amesema kuwa chama kitaendelea kuwahimiza
viongozi wake kutatua changamoto ndani ya jamii
Kwa upande wake Abdalla Omar Muya
Mwenyekiti wa ujenzi Skuli ya sekondari Kilindi amesema
msaada huo umefika muda mwafaka kwani utasaidia kumaliza changamoto
ya vyumba vya kusomea
0 Comments