HABARI MPYA

6/recent/ticker-posts

ACT Wazalendo washinda katika Uchaguzi mdogo jimbo la Pandani, CCM yaibuka mshindi wa pili

ZOEZI  LA kupiga kura uchaguzi Mdogo wa nafasi ya Uwakilishi  Jimbo la Pandani umemalizika  na kutangazwa matokeo  ambapo Prof Omary Fakih Hamad kutoka chama cha ACT wazalendo  ameibuka kidedea huku  akiwashinda wangombea  tisa   walio shiriki katika uchaguzi mdogo jimbo hilo.

Akitangaza matokeo ya uchaguzi Khamis Abdalla Hassan  afisa uchanguzi  mkoa wa kaskazini pemba  amesema kuwa Omar Fakih Hamad ameshinda kwa kura 2361  sawa na sailimia 52.5 huku akifatiwa na   Mgombea kupitia chama cha ccm Mohamed Juma Ali  alie pata kura  1934 sawa na aslimia 43.

Kwa upande wao walio shindwa katika uchaguzi huo  wameishukuru tume ya  uchaguzi kwa kwendesha zoezi hilo kwa huru na haki  na  kuwataka wanchi kushurikiana na mshindi alie patikana

 Jimbo la Mpandani linafanya Uchaguzi wa Mwakilishi kufuatia kifo cha aliyekuwa Mwakilishi Mteule wa Jimbo hilo Abubakar Khamis Bakari kupitia Chama cha ACT Wazalendo kufariki dunia, usiku wa kuamkia Novemba 11, 2020.

#UGATvFurahaYako


Post a Comment

1 Comments