HABARI MPYA

6/recent/ticker-posts

WADAU WA HABARI, WANDISHI WA HABARI ZANZIBAR BADO WANALIA NA SHERIA KANDAMIZI

 

+


NA Masanja Mabula -PEMBA

NI takribani robo karne imepita tangu  sheria ya Habari Zanzibar imefanyiwe mabadiliko ambayo hata hivyo bado hayajaleta suluhisho la changamoto zinazawakabili wandihsi wa habari

Kwa kipindi chote hicho wadau wa habari wakiwemo wandishi wa habari wamekuwa wakipiga chapuo kuomba sheria ambazo ni kandamizi ziweze kuondoshwa ili kutoa uhuru wa wanandishi na wadau wa habari kutumia vyema tasnia hiyo kwa lengo la kuleta mabadiliko chanya.

Kubadilishwa au kufanyia marekebisho sheria kandamizi ikiwemo ile ya Usajili na Uwakala wa Habari, Magezeti na Vitabu No/1988 ambayo ilifanyiwa marekebisho 1997 itatoa fursa na mawanda mapana kwa wadau na wandishi wa habari kutimiza malengo na wajibu kihabari.

Kupitia kifungu cha 30 cha sheria hii kimetoa mamlaka makubwa mno kwa Waziri wa Habari kuweza kuchukua maamuzi ya kukifungia na kusitisha kazi za chombo cha habari pasi na kuhitaji ushauri kutoka mamlaka nyengine.

Makala haya imefanya mahojiano na baadhi ya wandishi wa habari nguli , weledi na waboboezi wa tasnia ya habari Kisiwani Pemba ambao wametoa maoni yao juu ya sheria hii ambayo wamiitaja kuwa ni kikwazo cha maendeleo na uhuru wa wandishi wa habari.

Ali Massoud Kombo Meneja wa Kituo cha Redio Jamii Micheweni amebainisha kwamba Sheria hii sio tu kuwa nikandamizi bali pia inaviza maendeleo ya  habari nchini.

Katika mahojiano na Makala haya Ali Masoud Kombo anasema mabadiliko ya baadhi ya sheria ikiwemo sheria hii Usajili na Uwakala wa Habari, Magezeti na Vitabu No/1988 ambayo ilifanyiwa marekebisho 1997 ili iendane na maendeleo ya tasnia ya habari.

“Kwa sasa sisi wasimamizi wa vituo vya Redio za Kijamii kila siku tunaamka na kusikiliza vyombo vya habari kujua Waziri kama hajachukua maamuzi ya kusimamisha matangazo au kufungia vituo vyetu, yaani siku zote huwa sina amani huwa na hofu, kwani huwezi jua Waziri atamka vipi siku hiyo”alisisitiza.

Picha ni Essau Simon Kalukubila  mmiliki wa UGA MEDIA ambae pia ni mwandishi  wa habari na mtangazaji wa Radio Jamii Micheweni.

Naye Essau Simon Kalukubila Mmiliki wa UGA MEDIA,amesema sheria hii ni kongwe na ambayo ilitungwa kulingana na mahitaji ya wakati huo,kwa sasa inahitaji kufutwa baadhi ya vifungu ambavyo vinaonekana kuwa ni kandamizi.

“Tangu niingie kwenye tasnia ya habari, wandishi na wadau wa habari wanaendelea kupaza sauti zao kuziomba mamlaka husika kuzifanyia marekebisho  badhi ya sheria ikiwemo hii Usajili na Uwakala wa Habari, Magezeti na Vitabu No/1988 lakini zimeshindwa kufanyiwa marekebisho au sijui hawa wahusika wanainterest nazo”alihoji.

Naye Ali Khatib Chwaya Mwandishi wa Habari Mkongwe Kisiwani Pemba anasema mabadiliko yanahitajika kwani wakati sheria hii inatungwa ilikuwa sahihi kulingana na wakati huo kwa kuwa kulikuwa na vyombo vichache vya habari.

"Nyinyi wandishi wa habari mnaochipukia endeleeni kupaza sauti kuomba hichi kifungu ambacho  kinaviza  uhuru wa habari kiondoshwe ,jambo ambalo pia litawafanya muwe huru kutekeleza majukumu ya kuihabarisha jamii”alishauri.

Akizungumza na wandishi wa habari kwenye mafunzo ya Sheria ya Habari Mmiliki wa Blog ya Pemba Today Haji Nassor Mohammed amewataka kushirikiana katika kudai marekebisho ya sheria kandamizi zinazobinya uhuru wa wandishi.

Amesema zipo sheria nyingi ambazo zinaonekana kuwa shubili (chungu) kwa tasnia ya habari ikiwemo hii inayompa mamlaka waziri wa kufungia na kusitiza utoaji wa huduma (Kuhabarisha) kwa chombo cha habari.

“Mapambano haya tutashinda iwapo kila mmoja kwa kutumia chombo chake ataandika na kutangaza taarifa zinazotaka marekebisho ya sheria hii, itafika wakati wakubali na kuzirekebisha kama sio kuziondoa kabisa.

Mwandishi wa Makala haya binafsi nikiri kwamba mmoja wa wandishi wa habari Kisiwani Pemba ambaye anafaa kuungwa na mkono, ni Haji Nassor Mohammed ambaye amekuwa ni mfano wa kuigwa katika mapambano haya ya marekebisho ya sheria kandamizi.

Moja ya Makala yake na hapa  na nukuu “Kwa mfano, kifungu cha 27(2) cha Sheria ya Usajili wa Wakala wa Habari, Magazeti na Vitabu Na. 5 ya 1988,Kwa muktadha huo, kifungu cha maneno yaliyotumika yana utata ndani yake, maana hayaeleweki sawasawa kwa sababu kimekusanya maneno mengi na tata, yasiyofahamika”mwisho wa kunukuua

Kwa upande wake Hawra Shamte, mwandishi wa habari Mkongwe Visiwani hapa, akitoa mafunzo kwa wandishi wa habari katika Ofisi za Tamwa Pemba alisema kifungu hicho kinampa mamlaka waziri  kukifungia chombo cha habari pindi akiona yeye

“Hichi kifungu kinahitaji kuondohwa kwani kinakandamiza uhuru wa habari, kwani ni vigumu kuweza kubaini dhana na shuku, hivyo tunashauri kiondoshwe,” alisema.

Kwa upande wa wadau wa habari na kilio chao ni kwa sheria hii kwani wanasema ikiachwa iendelee kutumia inaweza kusababisha umaskini kwa jamii.

Mohammed Suleiman (Babu Eddy) mmiliki wa Rada Online TV, amesema kitendo cha waziri kupewa mamlaka makubwa na sheria ya kuweza kukifungia chombo chochote cha habari kinaweza kuwa ni sababu ya umaskini.

“Vijana wengi wamewekeza kwenye mitandao ya kijamii, hivyo waziri akiamka na kutoa maamuzi ya kufungia chombo cha habari itachangia umaskini kwani chombo kinategemewa na baadhi ya vijana kuendesha maisha yao”alisema.

Hata hivyo wandishi wa wadau wa habari wameshauri na kutoa mapembezo yafuatayo;-

Kabla ya waziri kuchukua maamuzi ya kukifungia chombo cha habari , anapaswa kushauriana na wadau wa habari ikiwemo BARAZA LA HABARI TANZANIA –MCT-pamoja na wadau wengine wa habari wakiwemo Vilabu vya wandishi wa habari na  TAMWA.    

Kuundwe bodi ambayo itakuwa na jukumu la kusimamia na kuratibu mwenendo wa vyombo vya habari.

 

Post a Comment

0 Comments